- 2,664 viewsDuration: 3:01Aliyekuwa mbunge wa lugari cyrus jirongo, alifariki kutokana na majeraha mabaya ya ndani yaliyotokana na ajali ya barabarani. Upasuaji wa maiti uliofanywa na kundi la wapasuaji umebaini kuwa kulikuwa na majeraha makubwa katika mbavu na mishipa ya damu inayozunguka moyo, iliyopelekea marehemu kuvuja damu kwa wingi kifuani. Hata hivyo, licha ya matokeo ya upasuaji wa maiti, maswali mengi bado yanaendelea kuzingira kifo hicho.