Wanajeshi 8 DRC wahukumiwa kifo kwa kukimbia vita
Mahakama ya kijeshi katika mji wa Goma huko Kivu Kaskazini Mashariki mwa Congo imewahukumu kifo maafisa nane wa jeshi la Congo, FARDC kwa tuhuma za kukimbia vita na kutoheshimu sheria za kijeshi.
Miongoni mwao ni Kanali Shamba mkuu wa kikosi cha makomandoo pamoja na msaidizi wake.
Mwendesha mashtaka amesema makamanda hao walishindwa kuwajibika kwenye uwanja wa mapambano karibu na mji wa Sake wilayani Masisi eneo lililo magharibi mwa mji wa Goma ambako M23 wanaendelea kuchukua udhibiti wa vijiji.
Wakili wa makamanda hao Bwito Jean Richard wa jeshi tiifu kwa serikali amesema mahakama imefanya makosa kutoa adhabu ya kifo kwa wanajeshi hao ambao walikuwa wamejitolea kulipigania taifa.
Hata hivyo amekata rufaa na kuionya Mahakama kuwa makini kwa kuwa hatua za mahakama zinaweza kuwapelekea wanajeshi wengi kutokwenda vitani.
Lakini baadhi ya wachambuzi wamesema hatua hii itawazuia wanajeshi kukimbia mapigano kila mara na kuwaacha waasi kuchukua vijiji.
Katika hukumu hiyo wanajeshi watatu, kapteni mmoja na maluteni wawili waliachiliwa huru na mahakama kwa madai ya kutokuwa na hatia.
Makamanda hao walipewa adhabu ya kifo kwa mujibu wa sheria ya nchi hiyo. Wakati huohuo Mkuu wa mahakama ameziomba pande husika kukata rufaa katika kipindi cha siku tano.
#mahakama #kijeshi #wanajeshi #hukumu #kifo #vita #voa #voaswahili #mahakamayakijeshi
Imeandaliwa na Austere Malivika , Sauti ya Amerika Goma
18 May 2024
- The shilling has strengthened against the Euro and the Sterling Pound by 18 per cent.
18 May 2024
- On Friday, 14 MPs from the Democratic Party accused the House Speaker of disrespecting Kenya.
18 May 2024
- Raila made his intention clear at a rally in Suna East, Migori County.
19 May 2024
- Hundreds of protesters in Peru's capital marched on Friday to demand the scrapping of a new law that describes transgender people, among others, as having a mental illness so they can access health benefits.
19 May 2024
- Israeli troops and tanks pushed on Saturday into parts of a congested northern Gaza Strip district that they had previously skirted in the more than seven-month-old war, killing and wounding dozens of Palestinians, medics and residents said.
19 May 2024
- Slovakia's health minister said Saturday the prognosis for Prime Minister Robert Fico was "positive" after an assassination attempt as a court put the suspected gunman in pre-trial detention.
19 May 2024
- Hundreds of residents from Cheptigit village in Kerio Valley will spend the night in the cold after the Kenya Wildlife Service (KWS) embarked on the demolition of houses for what it terms as encroachment.
19 May 2024
- The Orange Democratic Movement (ODM) party MPs have rallied to have the Azimio coalition shoot down the Finance Bill, 2024 terming it punitive and unbearable.
19 May 2024
- Police are investigating an incident in which a young man was shot dead during a violent confrontation between rival groups in Thika, Kiambu County, on Friday evening.
19 May 2024
- Gachagua expected to fight back after week of silence amid attacks
19 May 2024
- Police probe fatal shooting incident over market space dispute
19 May 2024
- 10,000 gather for Bohra spiritual leader's week-long celebrations
19 May 2024
- Firm charts green energy path with low-carbon emission engines