- 99 viewsKatika wiki za hivi karibuni, kikundi cha M23 kimerudi tena kwenye vichwa vya habari vya kimataifa kwa kuiteka Goma, mji muhimu upande mashariki mwa Congo. Lakini hawa ni nani (M23), na kwa nini kuibuka kwao upya kumechochea upinzani, ghasia na wasiwasi wa kimataifa? Haya ndiyo unapaswa kuyafahamu kuhusu M23, chimbuko lao, na mgogoro unaosambaa huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Kikundi cha waasi wa M23, au Harakati za Machi 23, zimepewa jina hilo kutokana na mkataba wa amani wa 2009 kati ya serikali ya Congo na kikundi cha waasi kinacho ongozwa na Watutsi, CNDP. Makubaliano hayo yaliahidi kuwaingiza waasi katika jeshi la taifa na ulinzi kwa jamii za Watutsi lakini halikutekelezwa kikamilifu, na kuzusha uasi wa M23 mwaka 2012. Licha ya kushindwa mwaka 2013, kikundi hicho kilirejea tena mwaka 2021, na kuchochea mgogoro huko mashariki mwa Congo. Wiki hii, M23 ilichukua udhibiti wa Goma, mji wenye watu takriban milioni 2 na kituo cha kibinadamu, ukiwemo uwanja wake wa ndege, na kukata njia muhimu za kufikisha misaada. Shambulizi hilo liliuwa watu kadhaa walioachwa mitaani, hospitali zilielemewa, na taarifa za uporaji na uvunjifu wa haki za binadamu. Maelfu wameukimbia mji huo, wakati waandamanaji mjini Kinshasa walishambulia balozi kadhaa za nchi ambazo zinazishutumu kuwa zinaisaidia M23, ikiwemo Rwanda. DRC inaishutumu Rwanda kwa kuisaidia M23 ili kunyakua utajiri wa madini yaliyoko katika kanda hiyo – madai ambayo yanakanushwa na Rwanda, licha ya ripoti za Umoja wa Mataifa kuunga mkono tuhuma za Congo. Mgogoro huo unaakisi vita kadhaa vya Congo huko nyuma, ambavyo viliuwa mamilioni na kuuyumbisha ukanda huo. Huku mivutano ikiongezeka, jumuiya ya kimataifa inahofia mgogoro huo unaweza kuongezeka kuwa vita vipana zaidi vya kanda hiyo, kuzidisha hali mbaya zaidi ya maafa ya kibinadamu na kutishia amani iliyo hatarini katika eneo la Maziwa Makuu. - VOA #voaswahili #afrika #rwanda #drc #m23 #dacs
Waasi wa M23 wanaopigana mashariki mwa Congo ni nani?
- - 🔴LIVE | TV47 MATUKIO ››
- 5 Feb 2025 - The European Union wants to engage swiftly with the United States over President Donald Trump's planned tariffs, trade chief Maros Sefcovic said on Tuesday, while his boss Ursula von der Leyen stressed the bloc would protect its interests in negotiations.
- 5 Feb 2025 - KMPDU has formally announced a strike by doctors at MTRH following what it terms as collapsed talks.
- 5 Feb 2025 - The government is taking decisive action to eradicate insecurity in the North Eastern region of Kenya, President William Ruto has said.
- 5 Feb 2025 - Five people were shot and wounded at a school in the central Swedish city of Orebro on Tuesday, police said, urging the public to stay away from the area as a large operation was underway.
- 5 Feb 2025 - Over 2,000 bodies require burial in Goma after Rwanda-backed M23 rebels took over the Democratic of Congo city last week, inflaming a decade-old conflict and humanitarian crisis, Congo's communications minister Patrick Muyaya said late on Monday.
- 5 Feb 2025 - Over 700 cases of maladministration by the judiciary have been reported in the last 5 years, with 60 percent of those cases yet to be resolved.
- 5 Feb 2025 - Heavily armed gangs in Haiti have attacked a neighborhood that's home to most of the country's elite and had been largely untouched by criminals, and police have demanded help repelling the assault that has killed at least 40 people.
- 4 Feb 2025 - The family of 19-year-old Elvis Munene is pleading with the government to help find their son after he went missing on January 29, under mysterious circumstances.
- 4 Feb 2025 - President William Ruto has pledged to bring back the five chiefs who were abducted by suspected Al-Shabaab militia on Monday in Mandera County, saying the country will not cede an inch to criminals.
- 4 Feb 2025 - He further alleged that MPs were given Sh500,000 each, while senators received Sh10 million to support his removal from office.