- 612 viewsDarzeni ya wanajeshi wa Congo wamewekwa kizuizini huko Bukavu, mji mkuu wa jimbo la Kivu Kusini, wakati mamlaka zikijiandaa kuwafungulia mashtaka wanajeshi wasiopungua 75 kwa kukimbia jeshini na vitendo vya ghasia dhidi ya raia, ikiwemo mauaji na uporaji. Kanda ya video kwenye mtandao wa kijamii iliyothibitishwa na Reuters Jumatatu (Februari 10) iliwaonyesha watu wakiwa na mavazi ya kiraia wakiingizwa kwenye Jela Kuu huko Bukavu. Mtazamaji katika kanda hiyo ya video aliwashutumu kuwa ni wanachama wa kikundi cha Cheetahs, kitengo cha jeshi la Congo, akisema “wanavuruga amani yetu.” Kuhusishwa kwa wafungwa katika video hiyo haukuweza kuthibitishwa na vyanzo huru. Reuters imethibitisha eneo hilo ni Bukavu kwa kulinganisha kuta za jela hiyo, lango kuu, miti yenye kuizunguka na milima na picha za satellite za eneo hilo. Wakati tarehe hasa ya kutolewa kanda hiyo ya video haikuweza kuthibitishwa na vyanzo huru, ilikuwa imepakuliwa kabla ya Jumatatu siku ya kesi. Chanzo cha jumuiya ya kiraia huko Kavumu, mji ulioko kilomita 35 kaskazini mwa Bukavu, ameiambia Reuters kuwa wanajeshi waliokimbia waliwauwa watu 10, wakiwemo saba kati yao waliokuwa wameketi baa Ijumaa jioni. Ofisi ya mwendesha mahtaka ya jeshi ilisema wanajeshi hao wanakabiliwa na mashtaka ya kukimbia kutoka mstari wa mbele baada ya waasi wa M23 kuuteka mji wa Nyabibwe, ulioko kilomita 70 kaskazini mwa Bukavu. Wanatuhumiwa pia kuhusika na ubakaji, mauaji, uporaji na uasi. (Reuters). #drc #congo #m23 #reels #voa
Wanaodaiwa kukimbia jeshini wawekwa jela kabla ya kesi kusikilizwa
- » Two foreigners among 4 arrested for running fake university, issuing bogus Masters and PhD degrees14 Feb 2025 - Four suspects have been arrested and arraigned for issuing irregular Master's and PhD degrees and operating a university without accreditation.
- 14 Feb 2025 - The Commission on Administrative Justice (CAJ) has asked the Director of Pensions to pay all pending 144 claims within 60 days, failure to which they will pursue means to declare him unfit to hold public office.
- 13 Feb 2025 - Kenya is staring at a condom shortage crisis following the funding freeze on United States Agency for International Development (USAID) programs.
- 13 Feb 2025 - The Southern African Development Community (SADC), comprising 16 member states, has officially urged its members to back Madagascar’s candidate in the African Union Commission (AUC) chairmanship elections set for Saturday, February 15.
- 13 Feb 2025 - Kenya Power said the interruption is part of network maintenance
- 13 Feb 2025 - In the judgment delivered Thursday, he has also been barred from holding public office.
- 13 Feb 2025 - Police say a driver drove into a crowd injuring at least 28 people
- 13 Feb 2025 - “Dynamics have changed in 2025; men are the prize now! If I don’t get anything, we move.”
- 13 Feb 2025 - "The accused persons entered a plea of not guilty where they were given bond of Sh400,000."
- 13 Feb 2025 - The Speaker said it is disheartening for legendary broadcaster Mambo Mbotela to be buried in Lang’ata Cemetery