- 8,486 viewsDarzeni ya wanajeshi wa Congo wamewekwa kizuizini huko Bukavu, mji mkuu wa jimbo la Kivu Kusini, wakati mamlaka zikijiandaa kuwafungulia mashtaka wanajeshi wasiopungua 75 kwa kukimbia jeshini na vitendo vya ghasia dhidi ya raia, ikiwemo mauaji na uporaji. Kanda ya video kwenye mtandao wa kijamii iliyothibitishwa na Reuters Jumatatu (Februari 10) iliwaonyesha watu wakiwa na mavazi ya kiraia wakiingizwa kwenye Jela Kuu huko Bukavu. Mtazamaji katika kanda hiyo ya video aliwashutumu kuwa ni wanachama wa kikundi cha Cheetahs, kitengo cha jeshi la Congo, akisema “wanavuruga amani yetu.” Kuhusishwa kwa wafungwa katika video hiyo haukuweza kuthibitishwa na vyanzo huru. Reuters imethibitisha eneo hilo ni Bukavu kwa kulinganisha kuta za jela hiyo, lango kuu, miti yenye kuizunguka na milima na picha za satellite za eneo hilo. Wakati tarehe hasa ya kutolewa kanda hiyo ya video haikuweza kuthibitishwa na vyanzo huru, ilikuwa imepakuliwa kabla ya Jumatatu siku ya kesi. Chanzo cha jumuiya ya kiraia huko Kavumu, mji ulioko kilomita 35 kaskazini mwa Bukavu, ameiambia Reuters kuwa wanajeshi waliokimbia waliwauwa watu 10, wakiwemo saba kati yao waliokuwa wameketi baa Ijumaa jioni. Ofisi ya mwendesha mahtaka ya jeshi ilisema wanajeshi hao wanakabiliwa na mashtaka ya kukimbia kutoka mstari wa mbele baada ya waasi wa M23 kuuteka mji wa Nyabibwe, ulioko kilomita 70 kaskazini mwa Bukavu. Wanatuhumiwa pia kuhusika na ubakaji, mauaji, uporaji na uasi. (Reuters). #drc #congo #m23 #reels #voa
Wanaodaiwa kukimbia jeshini wawekwa jela kabla ya kesi kusikilizwa
- - 🔴LIVE | TV47 MATUKIO ››
- 29 Apr 2025 - In a circular, Nyakango halted issuance of bursaries to learners by devolved units
- 29 Apr 2025 - Writhing in pain on a hospital bed in a Kenyan coastal town, teenage snakebite victim Shukurani Konde Tuva faced the grim reality of his left leg from above the knee being amputated.
- 29 Apr 2025 - A 25-year-old man drowned in the Thiba River while swimming at Rukenya Falls in Gichugu, Kirinyaga County, on Sunday.
- 29 Apr 2025 - Erin Patterson, 50, is charged with three murders -- including both of her parents-in-law -- and one attempted murder.
- 29 Apr 2025 - A conclave is the centuries-old election of a pope that derives its name from the Italian “con clave” (with a key) to underscore that cardinals are sequestered until they find a winner.
- 29 Apr 2025 - Kenyan authorities have blocked the screening of a BBC documentary exposing police officers who shot dead protestors at last year’s anti-tax demonstrations at Parliament buildings in Nairobi, the British broadcaster says.
- 29 Apr 2025 - The move comes ahead of a Trump rally planned for Tuesday night near Detroit to mark the president's first 100 days in office.
- 29 Apr 2025 - Seasoned radio host Edward Carey Kwach has died. According to family spokesperson Michael Okwiri, the established radio presenter died on Monday night while undergoing treatment for meningitis.
- 29 Apr 2025 - The attack left a journalist fighting for his life at a Nairobi hospital.
- 29 Apr 2025 - The expulsions last week from the southern state of Louisiana come as US President Donald Trump takes a hard-line approach to migration.