Makamu Rais Vance ahojiwa iwapo kukata msaada kwa Ukraine kunaipa nguvu Russia?
Baada ya mkutano wa Ijumaa iliyopita kati ya Rais Donald Trump na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy ambao uligeuka malumbano makali, na Rais Tump kusitisha kwa muda misaada ya kijeshi kwenda Ukraine, Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance ameweka wazi msimamo wa Marekani kuhusu kumaliza vita vya miaka mitatu kati ya Russia na Ukraine.
Katika mahojiano na VOA, JD Vance aliulizwa ikiwa kusimamisha misaada kwa Ukraine kunaipa fursa nzuri Russia.
Vance amesema lengo la Rais Donald Trump kuhusu sera ya Marekani kwa Ukraine ni kuwaleta raia wa nchi hiyo kwenye meza ya mazungumzo.
Amesema wanataka Waukraine wawe na nchi inayojitawala na huru, akiongeza kuwa majeshi ya Ukraine yamepigana kwa ujasiri mkubwa, lakini wamefikia mahali ambako si Ulaya wala Marekani ambao wanaweza kuendeleza vita hivyo bila ya ukomo.
Ima kuhusu iwapo Marekani inaweza kufikia makubaliano ya madini na Ukraine wakati huu, Vance amesema ana imani makubaliano hayo yanaweza kufikiwa.
“Nafikiri Rais Trump bado ana azma ya kufikia makubaliano ya madini, na makubaliano hayo ni sehemu muhimu sana ya sera yake.”
Vance ameendelea kusisitiza kwamba wananchi wa Marekani wanastahili malipo kidogo ya uwekezaji mkubwa wa kifedha uliofanywa kwa Ukraine.
Kuhusu madai kwamba Marekani inaiwekea shinikizo kubwa Ukraine kuliko Russia na kwamba watu wanaweza kutarajia vikwazo zaidi vya Marekani dhidi ya Russia:
Makamu wa Rais Vance amesema halitakuwa jambo sahihi, akisema wanaamini msimamo wa Rais Trump ni kwa maslahi ya Russia, lakini pia kwa maslahi ya Ukraine na kwa maslahi mazuri ya Marekani kumaliza mgogoro huo.
#trump #zelenskyy #ukraine #russia #voa #makamurais #jdvance #msaada
6 Mar 2025
- CS Justin Muturi has for some time been at a crossroads with the Kenya Kwanza government.
6 Mar 2025
- The government will also be retraining all health workers across the country on how to operate the SHA portal to ensure efficiency.
6 Mar 2025
- This comes after a report circulated online claiming that the Judiciary misused the money.
6 Mar 2025
- Faith-based health facilities have issued a 14-day ultimatum for the government to clear their claims; failure to which they will not offer services to patients seeking the services using the Social Health Authority (SHA) and result on cash services only.
6 Mar 2025
- Reactions have flooded in after Inooro TV, on their popular Njeraini Citu program, aired the story of a young woman who was arrested and subsequently jailed for gambling away Ksh. 200,000 - money she had been entrusted to keep as an informal Sacco…
6 Mar 2025
- Edward Mwai, the founder of Jesus Winner Ministry, has cleared the air on allegations of land-grabbing to erect a church.
6 Mar 2025
- A road accident at Kolol area along the Iten-Kabarnet road left 12 people injured Thursday morning after a matatu veered off the road due to brake failure.
6 Mar 2025
- Notable individuals have been shortlisted for the positions of chairperson of the Independent Electoral and Boundaries Commission (IEBC).
6 Mar 2025
- Kenyan Ambassador to Thailand Kiptiness Lindsay Kimwole has revealed that 129 Kenyans rescued from Myanmar are now stuck at the Thailand border
6 Mar 2025
- Muslima Abdi, a well-wisher who took him to the hospital, described Nura’s difficult background, highlighting the lack of support he faced in overcoming drug addiction, which ultimately led to his mental health issues.
6 Mar 2025
- CS Justin Muturi has for some time been at a crossroads with the Kenya Kwanza government.
6 Mar 2025
- The government will also be retraining all health workers across the country on how to operate the SHA portal to ensure efficiency.
6 Mar 2025
- The ties will enhance mutual growth between the two countries.