- 371 viewsDuration: 2:57Idadi kubwa zaidi ya wanafunzi imeratibiwa kufanya mitihani ya taifa mwaka huu. Wanafunzi zaidi ya milioni 3.4 wakiwemo wale wa kidato cha nne, wa gredi ya sita na gredi ya tisa chini ya mtaala wa cbe, watafanya mitihani hiyo itakayoanza tarehe kumi na saba mwezi huu wa Oktoba. Na kama anavyoarifu Emily Chebet, baraza la mitihani -knec- imewaonya wazazi, walimu na wanafunzi dhidi ya ulaghai wakati wa mitihani.