Moto, milipuko yamulika angani kaskazini Israel Hezbollah iliposhambulia
Majeshi ya Israeli yamefanya mashambulizi ya angani Jumatano kusini mwa Lebanon katika mashambulizi ya hivi karibuni yanayolenga wanamgambo wa Hezbollah wakati kikundi cha Hezbollah cha Lebanon kilipoishambulia Julai 15 kwa makombora ambayo mifumo ya ulinzi wa anga ya Israel iliyatungua katika mji wa Kiryat Shmona.
Jeshi la Israel lilisema mashambulizi yake yalilenga miundombinu ya Hezbollah, na kwamba majeshi ya Israeli pia yalitumia makombora kujibu vitisho vya Hezbollah katika eneo hilo.
Hezbollah ilifyatua makombora kuelekea Israel, huku jeshi la Israeli likisema limezuia baadhi ya makombora hayo wakati mengine yalianguka katika eneo la wazi bila ya kuleta uharibifu au vifo.
Kiongozi wa Hezbollah Sayyed Hassan Nasrallah alisema wakati akitoa hotuba Jumatano kuwa kikundi cha wanamgambo hao watalenga maeneo mapya ndani ya Israel iwapo majeshi ya Israeli yataendelea kuua raia.
Shambulizi lililofanywa na Israeli Jumanne liliuua raia watano wa Syria huko kusini mwa Lebanon.
Mapigano ya mpakani kati ya Israel na Hezbollah yameongeza wasiwasi kuhusu mgogoro mkubwa zaidi kuzuka katika kanda hiyo huku majeshi ya Israeli yakiwa pia yanapigana na Hamas ndani ya Ukanda wa Gaza.
Waziri wa Ulinzi wa Marekani Lloyd Austin na Waziri wa Ulinzi wa Israeli Yoav Gallant walijadili mapigano yanayo endelea kati ya Israel na Hezbollah wakati wa mazungumzo waliofanya kwa njia ya simu Jumanne, Wizara ya Ulinzi ya Marekani ilieleza.
Msemaji wa Pentagon Major General Pat Ryder alisema katika taarifa yake kuwa mawaziri hao wa ulinzi pia walizungumzia kuhusu kivuko cha muda kilichojengwa na Marekani katika pwani ya Gaza ili kuwezesha misaada ya kibinadamu kuwafikia raia wa Palestina. -AFP, Reuters
#Rafah #Netanyahu #Misri #Hamas #Gaza #Palestina #IDF #GalMeirEizenkot #mauaji #jeshi #israel #voa #voaswahili #mwandishi #aljazeera #maghazi #wahouthi #marekani #uingereza #shambulizi #dhamar #yemen #hospitali #nasserhospital #lebanon #hezbollah #wanamgambo
22 Apr 2025
- Kenyan men have been accused of adopting outdated toxic traits.
22 Apr 2025
- Kenya's exports to the US are estimated at around Ksh109.7 billion (784 million USD).
22 Apr 2025
- The DCI revealed the case was escalated to the special unit.
23 Apr 2025
- Pope Francis' funeral will be held on Saturday in St. Peter's Square, Roman Catholic cardinals decided on Tuesday, setting the stage for a solemn ceremony that will draw leaders from around the world.
22 Apr 2025
- Easter holiday turned tragic for a family after their 6-year-old son died in a swimming pool at the Sun and Sand Hotel in Kikambala, Kilifi County.
22 Apr 2025
- Even as the more than 1.4 billion Roman Catholics around the world continue to mourn Pope Francis, speculation is building as to who among the 135 red-robed cardinals eligible to vote will succeed him.
22 Apr 2025
- The Controller of Budget (CoB) has raised a red flag over a growing financial indiscipline in counties that she says is exposing taxpayers' money to pilferage.
22 Apr 2025
- President William Ruto has arrived in China for a four-day State Visit at the invitation of His Excellency President Xi Jinping.
22 Apr 2025
- Six people have died overnight in Nairobi following heavy rains. Three of them—a mother and her two children—were killed when a boulder crushed their house in Mathare.
22 Apr 2025
- The DCI has taken over the probe into alleged human organ trafficking at Mediheal Hospital’s Fertility and Transplant Centre in Eldoret, Uasin Gishu County.
22 Apr 2025
- The gunmen fired indiscriminately at the convoy.
22 Apr 2025
- Four individuals have been charged at the Milimani Law Courts with conspiracy to defraud different businessmen by falsely claiming they could import sugar from Brazil to Kenya.
22 Apr 2025
- A case that has captured both national and international attention is set to resume on Wednesday at the Jomo Kenyatta International Airport (JKIA) Law Courts, where four suspects stand accused in Kenya’s first major prosecution under the Nagoya Protocol…