WAHAMIAJI NANE WAFARIKI WAKIJARIBU KUELEKEA UINGEREZA

  • | VOA Swahili
    417 views
    Wahamiaji nane wamekufa Jumapili wakati boti yao iliyokuwa imejaa watu zaidi ya uwezo wake kuzama ikijaribu kuvuka bahari ya English Channel kutoka Ufaransa kuelekea Uingereza maafisa wa usalama wa Ufaransa wamesema. Ajali hii imetokea chini ya wiki mbili baada ya maafa mabaya zaidi kama hayo kutokea mwaka huu. Tukio hilo baya linamaanisha idadi ya waliofariki kutaka kuelekea Uingereza kutoka Ufaransa imeongezeka kufikia wahamiaji 46 kutoka 12 waliofariki mwaka 2023, ambao wamepoteza maisha yao wakijaribu kuingia Uingereza kutoka Ufaransa, afisa wa jimbo amesema. Serikali za Ufaransa na Uingereza zimepambana kwa miaka kadhaa kusitisha wimbi la wahamiaji ambao wanalipa wasafirishaji haramu maelfu ya Euro kila mtu kwa ajili ya kuvuka kwa boti zilizojaa watu kupita kiasi. Watu sita walionusurika wamelazwa hospitali akiwemo mtoto wa miezi 10 mwenye matatizo ya afya kutokana na baridi kali. - AFP #wahamiaji #uingereza #englishchannel #bahari #ufaransa #ajali #boti #voa #voaswahili