Baraza la wazee lamtaka Ruto kuzima mchakato wa kumuondoa Gachagua

  • | Citizen TV
    2,206 views

    Baraza la wazee linamtaka Rais William Ruto kuingilia kati na kusitisha mchakato wa kumwondoa ofisini naibu Rais Rigathi Gachagua. Baraza hilo linasema kuwa pilkapilka hizo hazina umuhimu mkubwa kwa wananchi. Wakiwarai rais na naibu wake kuzungumza na kutatua masuala yanayowakosanisha, wazee hao wamemtaka rais kufanya kipaumbele masuala yanayowahusu wakenya kama vila bima ya maisha, gharama ya maisha, ufadhili wa wanafunzi wa vyuo vikuu na kadhalika.