Mshindi wa maonyesho ya urembo ya mwaka wa 2025 barani Afrika ni Accelle Dillar kutoka nchini Chad baada ya kuibuka mshindi kwenye maonyesho ya urembo yaliowashirikisha warembo 16 kutoka mataifa mbalimbali ya bara Afrika. Kutokana na ushindi huo, atakabidhiwa dola alfu tano za Marekani miongoni mwa zawadi nyingine. Akihudhuria hafla hiyo, mkurugenzi wa maswala ya mipango ya kimkakati kwenye tume ya filamu nchini, Collins Okoth , alisema kama mojawapo ya hatua za kukuza sekta ya ubunifu, tume hiyo pamoja na mashirika mengine ya serikali, yataweka mipango ya kuimarisha ubunifu pamoja na kubuni nafasi za kibiashara .
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive