- 136 viewsMajeshi ya Israeli yaliondoka kutoka katika mji wa Palestina wa Jenin Ijumaa (Septemba 6), wakiacha athari za uharibifu mkubwa wa majumba na miundombinu, kufuatia moja ya operesheni kubwa kabisa ya kiusalama katika eneo ambalo limekuwa likikaliwa kwa mabavu huko Ukingo wa Magharibi kwa miezi kadhaa. Akihojiwa kuhusu madai ya kuwa eneo hilo lina maghaidi, Samaher Abu Nassa, mkaazi wa eneo hilo la Jenin alisema: Hapana, sisi siyo magaidi, sisi ni watu wa amani. Wao ndiyo magaidi, wanawauwa watoto wetu.” Jeshi la Israeli lilisema operesheni hiyo ililenga kuzuia vikundi vya wanamgambo vinavyoungwa mkono na Iran kupanga mashambulizi dhidi ya raia wa Israeli. Limesema kuwa majeshi ya Israeli yamewauwa wanamgambo 14 wakati wa operesheni hiyo, ikiwemo makamanda wa eneo wa Hamas huko Jenin. Siku ya Ijumaa, maelfu walijiunga katika maziko kuwapeleka makaburini wale waliouwawa wakati wa mapigano. Wakati majeshi ya Israeli yalijikita hasa katika sehemu kubwa ya mwaka uliopita huko Gaza, Ukingo wa Magharibi umeshuhudia kuongezeka ghasia. Zaidi ya Wapalestina 680 wameuwawa huko Ukingo wa Magharibi na East Jerusalem, kulingana na wizara ya afya ya Palestina. #voaswahili #afrika #hezbollah #israel #hamas #fatah #iran #islamicjihad #watoto #vifo #jenin #gaza
Majeshi ya Israeli yaacha athari za uharibifu Jenin
- 22 Apr 2025 - Pope Francis died of a stroke, causing a coma and "irreversible" heart failure, according to his death certificate released by the Vatican on Monday.
- 22 Apr 2025 - Nairobi City Thunder (NCT) basketball team has received a major boost ahead of the upcoming Basketball Africa League (BAL) championship, after being assigned a Senegalese NBA G-League player to reinforce the squad. The team is also eyeing continental…
- 22 Apr 2025 - The papacy journey started with St. Peter, he who Christ christened as the rock of the Church.
- 22 Apr 2025 - Tragedy struck on Monday at Loberer area along the Marigat-Chemolingot route in Baringo County, where two people were shot dead and two others injured. The victims were ambushed by suspected bandits while travelling to Nginyang market in a police convoy…
- 22 Apr 2025 - Kenya Chipu aim to defend Barthes Trophy after perfect start
- 22 Apr 2025 - People's Pope signs off, leaving behind a church changed forever
- 22 Apr 2025 - From social justice to tackling abuse: 12 years of Pope Francis
- 22 Apr 2025 - Role of Commissioner for Cooperatives questioned in Kuscco Sh13b saga
- 22 Apr 2025 - Youths dare dream as Nyanza's Junior Golf tourney highlights growth
- 22 Apr 2025 - The inconvenient truth about devolution, the environment