- 1,704 viewsDuration: 3:58Siku nne baada ya mwanaharakati Bob Njangi na rafikiye Nicholas Oyoo kutekwa nyara nchini Uganda, mwenzao aliyeponyoka, Koffi Atinda anaelezea matukio hayo. Koffi aliwasili humu nchini Jumamosi baada ya changamoto nyingi nchini Uganda na anadai kuwa waliomteka nyara walikuwa wamevaa sare za polisi huku wakiwa wamebeba bunduki. Ode Francis alizungumza naye na kutayarisha taarifa ifuatayo