Katika hotuba ya rambirambi iliyojaa msisimko, Ida Odinga mjane wa marehemu aliyekuwa waziri mkuu Raila Odinga alimwomboleza mumewe akisema alikuwa mwanamume mwenye wingi wa msamaha ambaye alipenda na kujitolea kuihudumia familia yake na taifa kwa jumla. Katika hafla ya ibada ya mazishi kwenye uwanja wa chuo kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Oginga Odinga kaunti ya Siaya iliyohudhuriwa na watu mashuhuri, viongozi wa kisiasa na maelfu ya wakenya, Ida alichora taswira ya maisha ya mwanamume ambaye maisha yake yalihusu kujitolea, ustahilivu na imani isiyotetereka kwa ajili ya taifa bora.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive