Mwanaharakati wa kutetea haki za binadamu ambaye pia alitangaza azma ya kuwania urais Boniface Mwangi, ameelezea wasiwasi wake kuhusu kile anachodai kuwa majaribio ya kumtishia maisha. Mwangi, ambaye amekuwa mkosoaji mkubwa wa serikali, amedai tukio la hivi majuzi katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Jomo Kenyatta ni la kutisha, baada ya kudai kwamba alipata ganda la risasi kwenye sanduku lake muda mfupi kabla ya ndege yake kuondoka. Mwangi amesema tukio hilo ni mojawapo wa misururu ya matukio yanayolenga kuwanyamazisha wakosoaji, huku akiahidi kuendeleza azma yake ya kisiasa.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive