- 219 viewsPolisi wa Uganda wamesema Jumapili kuwa idadi ya vifo kutokana na maporomoko ya ardhi kwenye eneo kubwa la kutupia taka mjini Kampala imefikia 21, wakati timu za uokozi zikiendelea kutafuta manusura na idadi ya miili inayopatikana ikielekea kuongezeka. Kwa mujibu wa shirika la habari, mvua kubwa ambazo zimekuwa zikinyesha katika wiki za karibuni zilisababisha kuporomoka kwa sehemu ya eneo hilo, ambalo ndilo pekee linalotumika kutupa takataka mjini humo, na kupelekea kufunikwa kwa baadhi ya nyumba zilizokuwa karibu, wakati wenyewe walipokuwa wamelala. Mamlaka za jiji Jumamosi zilisema kuwa watu 8 walikufa, lakini kufikia leo idadi hiyo imeongezeka hadi 21, huku wengine 14 walijeruhiwa. Kati ya waliofariki miili isiyopungua miwili ilikuwa ya watoto. Shirika la Msalaba mwekundu nchini humo limesema kuwa mahema yamewekwa karibu na eneo la tukio, ili kutoa hifadhi kwa watu walioathiriwa. Eneo hilo linalofahamika kama Kiteezi, kwa miongo mingi limekuwa likitupwa taka taka za Kampala, hadi kugeuka na kuwa mlima, huku wakazi waishio karibu wakilalamika kutokana na taka zenye sumu, pamoja na uharibifu wa mazingira. Nchini Ethiopia, takriban watu 115 walikufa 2017 baada ya eneo la taka mjini Addis Ababa kuporomoka, huku wengine 17 wakifa 2018, mjini Maputo, Msumbiji, kwenye tukio sawa na hilo. – Reuters, AP, VOA #uganda #kampala #takataka #dumpo #maporomoko #vifo #polisi #voa #voaswahili
Idadi ya vifo katika eneo la kutupia takataka vyafikia 21
- - Hatima ya Gachagua ››
- 23 Oct 2024 - Four senior Taita Taveta County officials arrested on Tuesday over the alleged theft of Ksh.7 million public funds in the pretext of commemorating the First World War are due in court on Wednesday.
- 23 Oct 2024 - The Kenyan Network of Cancer Organizations (KENCO) and Cancer Survivors Association of Kenya have united to petition the government to restore full access to cancer treatment services.
- 23 Oct 2024 - Israel on Tuesday confirmed it had killed Hashem Safieddine, the heir apparent to late Hezbollah leader Hassan Nasrallah who was killed last month in an Israeli attack targeting the Iran-backed Lebanese militant group.
- 23 Oct 2024 - A one-year-old child died while 14 passengers were hospitalised in serious condition after a truck rammed into a matatu along the Narok-Maimahiu road in the Pinyinyi area of Narok County on Tuesday night.
- 23 Oct 2024 - A one-year-old child died while 14 passengers were hospitalised in serious condition after a truck rammed into a matatu along the Narok-Maimahiu road in the Pinyinyi area of Narok County on Tuesday night.
- 23 Oct 2024 - The E. coli outbreak, linked to one of McDonald's most popular menu items, has sickened 49 people and sent 10 to the hospital, officials say.
- 23 Oct 2024 - The youngster aced her competitors to win the award.
- 23 Oct 2024 - Hashem's prominence grew during recent conflicts, notably addressing rallies and showing support for Hamas during the Gaza war.
- 23 Oct 2024 - JPMorgan Chase CEO Jamie Dimon remains cautious about publicly expressing this possibility.
- 23 Oct 2024 - Parents face mounting costs as exams season draws