Serikali ya Kajiado na ya kitaifa zasitisha ugavi wa shamba la Malisho la Rombo

  • | Citizen TV
    454 views

    Serikali ya Kitaifa na Ile la Kaunti ya Kajiado zimepiga marufuku shughuli zozote za Ugavi wa shamba la Malisho la Rombo ambao uliendeshwa miaka mitatu iliyopita na hata hati miliki kutolewa kwa wanachama zaidi ya Elfu Sita hadi pale mahakama itatoa uamuzi wake. Wakitoa Tangazo hilo Kwenye mkutano ulioandaliwa kwenye shamba hilo lenye ekari elfu 94,500, Kamishana wa Kajiado James Taari na Gavana wa Kaunti hiyo Joseph Ole Lenku wanasema kumekuwa na hali ya wasi wasi baada ya baadhi ya wanachama kuhisi wamedhulumiwa na sasa shuguli zote zitasimama hadi pale mahakama itatoa mwelekeo.