- 852 viewsRais wa Kenya William Ruto Ijumaa alimteua waziri wa mambo ya ndani Kithure Kindiki kuwa naibu wake mpya, siku moja baada ya baraza la Seneti kupiga kura ya kumtimua naibu wake wa zamani, Rigathi Gachagua. “Nimepokea ujumbe kutoka kwa rais, kuhusu kuteuliwa kwa Profesa Kithure Kindiki kushika nafasi hiyo ambayo imetokea afisini,” Spika wa bunge la kitaifa Moses Wetang’ula alisema Ijumaa, akiwahutubia wabunge mjini Nairobi. Gachagua, ambaye alikanusha mashtaka yote dhidi yake wakati wa kesi ya kuondolewa madarakani, alimuunga mkono Ruto katika ushindi wake wa 2022 na kusaidia kupatikana kwa kura nyingi kutoka eneo lenye wakazi wengi la kati mwa Kenya. Lakini katika miezi ya hivi karibuni , Gachagua amezungumza kuhusu kutengwa, huku kukiwa na taarifa zilizoenea kwenye vyombo vya habari kuwa ametofautiana na Ruto wakati miungano ya kisiasa ikibadilika. Kindiki, mshirika wa karibu wa Ruto, ameshikilia wadhifa wa wizara ya mambo ya ndani katika kipindi chote cha miaka miwili ya Ruto kama rais. Hapo awali aliwahi kuwa seneta wa Kaunti ya Tharaka Nithi na alikuwa mgombeaji mkuu kuwa mgombea mwenza wa Ruto wakati wa uchaguzi wa 2022. Baadaye Bunge litalazimika kupiga kura kuidhinisha uteuzi wa Kindiki kabla ya kuapishwa. #Kenya #seneti #gachagua #kindiki #voa #voaswahili
'Nawaunga mkono wabunge na seneti kwa muelekeo wao...'
- 21 Apr 2025 - Some cardinals who are being talked about as "papabili" to succeed Pope Francis, whose death at the age of 88 was announced by the Vatican on Monday.
- 21 Apr 2025 - The Vatican, headquarters of the Catholic Church, is the smallest state in the world, with its own newspaper, national anthem in Latin and supreme leader -- the pope.
- 21 Apr 2025 - African leaders praised the "legacy of compassion" and "commitment to inclusivity" of Pope Francis as they joined global mourning over his death on Monday.
- 21 Apr 2025 - South Sudan's army said it had recaptured a key town in Upper Nile state that it lost to an ethnic Nuer militia in March in clashes which led to the arrest of First Vice President Riek Machar and a spiralling political crisis.
- 21 Apr 2025 - Former President Uhuru Kenyatta has joined leaders and catholic faithful worldwide in mourning Pope Francis who passed on early this morning.
- 21 Apr 2025 - A hush reigned over the normally boisterous St Peter's Square on Monday as the faithful and the curious alike gathered at the seat of Catholicism to mark the death of Pope Francis.
- 21 Apr 2025 - Twenty-three bombs have been found underground in holes dug by residents of Hellu village, Moyale constituency, Marsabit county.
- 21 Apr 2025 - PS Sing'oei said Kenya hopes to move away from conventional loan arrangements.
- 21 Apr 2025 - The Eiffel Tower's landmark illuminations will be switched off on Monday night in memory of Pope Francis who died aged 88, Paris mayor Anne Hidalgo said.
- 21 Apr 2025 - Sunday's scheduled canonisation of the Catholic Church's first millennial saint has been postponed to a later date after the death of Pope Francis, the Vatican said on Monday.