Angola yasema itajaribu kusimamia mazungumzo kati ya DRC na M23
Angola imesema siku ya Jumanne itajaribu kusimamia mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda katika siku zijazo.
Haikufahamika iwapo serikali ya Congo, ambayo ilikataa mara nyingi kufanya mazungumzo na M23, itashiriki katika mazungumzo hayo.
Msemaji wa ofisi ya rais wa Congo aliiambia Reuters mamlaka hiyo imezingatia hatua hiyo, wakati naibu msemaji wa M23 alisema ulikuwa “ni ushindi wa hoja” na kuthibitisha ushiriki wa kikundi hicho katika mazungumzo hayo.
Rais wa DRC Felix Tshisekedi alifanya ziara ya kikazi mjini Luanda na alikutana na mwenzie Joao Lourenco, ofisi ya rais wa Angola ilisema katika taarifa kwenye Facebook.
“Angola kama mpatanishi katika mzozo wa mashariki mwa Congo, itaanzisha mawasiliano na M23, ili wajumbe kutoka Congo na M23 wafanye mazungumzo ya moja kwa moja mjini Luanda katika siku zijazo,” ofisi ya rais iliongeza.
Nchi hiyo iliyoko Kusini mwa Afrika imekuwa ikijaribu kusimamia kufikiwa kwa sitisho la mapigano na kupunguza mivutano kati ya Congo na jirani yake Rwanda, ambayo imekuwa ikishutumiwa kuwasaidia kikundi cha waasi wa Kitutsi.
Rwanda imekanusha kuwapa msaada wa silaha na wanajeshi waasi wa M23, na imesema majeshi yake yanajihami dhidi ya jeshi la Congo na wanamgambo wenye chuki na Kigali.
Waasi wa M23 wamekamata miji mikubwa miwili iliyoko mashariki mwa Congo tangu Januari katika mvutano wa mgogoro wa muda mrefu ambao kiini chake ulisambaa Congo kutokana na mauaji ya halaiki ya Rwanda yam waka 1994 na juhudi ya kutaka kudhibiti eneo kubwa lenye madini nchini Congo.
#angola #waasi #m23 #congo #felixtshisekedi #JoaoLourenco #rwanda
12 Mar 2025
- Businesses were left counting losses after attacks from rowdy youth.
12 Mar 2025
- Kenya was instrumental in the creation of South Sudan in 2011 and remains a leading partner for the world's youngest nation.
12 Mar 2025
- The company employs more than 1,500 people, and its operations generate 20,000 indirect jobs.
13 Mar 2025
- Prince William will visit Estonia on March 20 and 21, where he will meet with British troops deployed as part of NATO's deterrent against potential Russian aggression, Kensington Palace announced Wednesday.
13 Mar 2025
- Public Service Cabinet Secretary (CS) Justin Muturi has explained his recent absences from Cabinet meetings, stating that he requested to be excused from the meetings unless the issues of police abductions and extrajudicial killings were on the agenda.
13 Mar 2025
- Public Service Cabinet Secretary Justin Muturi has dismissed calls by a section of government leaders asking him to step down.
13 Mar 2025
- Eighteen people were arrested in Eastleigh, Nairobi County in a major crackdown by Kenya Revenue Authority (KRA) sleuths over dumping of goods in the country. The suspects are linked to a ‘well-deliberated’ complex tax evasion scheme of ‘cargo dumping’…
13 Mar 2025
- After 30 days in detention, murder suspect Elvis Kibiwot Torotoich was back in court as Juja detectives presented him before Lady Justice Florence Muchemi.
13 Mar 2025
- PS pledges to rebuild public trust in police
13 Mar 2025
- Nyoro, his ousted team accused of skewed sharing of 'budget' kitty
13 Mar 2025
- Court warns woman to keep daughter in forced marriage row
13 Mar 2025
- Involve youths in policy policy reforms to tackle skills mismatch, unemployment
13 Mar 2025
- How Kuscco board pocketed Sh18m for site visits to housing project