- 219 viewsPolisi wa Uganda wamesema Jumapili kuwa idadi ya vifo kutokana na maporomoko ya ardhi kwenye eneo kubwa la kutupia taka mjini Kampala imefikia 21, wakati timu za uokozi zikiendelea kutafuta manusura na idadi ya miili inayopatikana ikielekea kuongezeka. Kwa mujibu wa shirika la habari, mvua kubwa ambazo zimekuwa zikinyesha katika wiki za karibuni zilisababisha kuporomoka kwa sehemu ya eneo hilo, ambalo ndilo pekee linalotumika kutupa takataka mjini humo, na kupelekea kufunikwa kwa baadhi ya nyumba zilizokuwa karibu, wakati wenyewe walipokuwa wamelala. Mamlaka za jiji Jumamosi zilisema kuwa watu 8 walikufa, lakini kufikia leo idadi hiyo imeongezeka hadi 21, huku wengine 14 walijeruhiwa. Kati ya waliofariki miili isiyopungua miwili ilikuwa ya watoto. Shirika la Msalaba mwekundu nchini humo limesema kuwa mahema yamewekwa karibu na eneo la tukio, ili kutoa hifadhi kwa watu walioathiriwa. Eneo hilo linalofahamika kama Kiteezi, kwa miongo mingi limekuwa likitupwa taka taka za Kampala, hadi kugeuka na kuwa mlima, huku wakazi waishio karibu wakilalamika kutokana na taka zenye sumu, pamoja na uharibifu wa mazingira. Nchini Ethiopia, takriban watu 115 walikufa 2017 baada ya eneo la taka mjini Addis Ababa kuporomoka, huku wengine 17 wakifa 2018, mjini Maputo, Msumbiji, kwenye tukio sawa na hilo. – Reuters, AP, VOA #uganda #kampala #takataka #dumpo #maporomoko #vifo #polisi #voa #voaswahili
Idadi ya vifo katika eneo la kutupia takataka vyafikia 21
- - Duniani Leo ››
- 22 Apr 2025 - A little outreach goes a long way in redeeming lives of despised and shunned lot
- 22 Apr 2025 - Religious leaders say they are only holding Ruto accountable as head of state.
- 22 Apr 2025 - His tenure is not without challenges amid high expectations from taxpayers.
- 22 Apr 2025 - Court of Appeal upheld a High Court verdict that his intentional killing of an innocent man was inexcusable.
- 22 Apr 2025 - The current doctor-to-patient ratio in Kenya is still far below WHO recommendation of one doctor to 1,000 patients.
- 22 Apr 2025 - Nassir said the most difficult part was not bringing the building down, but the evacuation of 60,000 people.
- 22 Apr 2025 - Kenya’s hopes of qualifying for the 2025 Toyota Junior Golf World Cup in Japan now rest on the shoulders of seven rising golf stars who were officially flagged off yesterday at the Royal Nairobi Golf Club ahead of the All Africa Junior Team Championship…
- 22 Apr 2025 - With his storm of tariffs on Chinese goods, US President Donald Trump has torched ties with Beijing and likely wrecked any hope of meeting his counterpart Xi Jinping in the near term, analysts say. Ali Wyne, a senior research and advocacy adviser…
- 22 Apr 2025 - Pope Francis died of a stroke, causing a coma and "irreversible" heart failure, according to his death certificate released by the Vatican on Monday.
- 22 Apr 2025 - Nairobi City Thunder (NCT) basketball team has received a major boost ahead of the upcoming Basketball Africa League (BAL) championship, after being assigned a Senegalese NBA G-League player to reinforce the squad. The team is also eyeing continental…