- 219 viewsPolisi wa Uganda wamesema Jumapili kuwa idadi ya vifo kutokana na maporomoko ya ardhi kwenye eneo kubwa la kutupia taka mjini Kampala imefikia 21, wakati timu za uokozi zikiendelea kutafuta manusura na idadi ya miili inayopatikana ikielekea kuongezeka. Kwa mujibu wa shirika la habari, mvua kubwa ambazo zimekuwa zikinyesha katika wiki za karibuni zilisababisha kuporomoka kwa sehemu ya eneo hilo, ambalo ndilo pekee linalotumika kutupa takataka mjini humo, na kupelekea kufunikwa kwa baadhi ya nyumba zilizokuwa karibu, wakati wenyewe walipokuwa wamelala. Mamlaka za jiji Jumamosi zilisema kuwa watu 8 walikufa, lakini kufikia leo idadi hiyo imeongezeka hadi 21, huku wengine 14 walijeruhiwa. Kati ya waliofariki miili isiyopungua miwili ilikuwa ya watoto. Shirika la Msalaba mwekundu nchini humo limesema kuwa mahema yamewekwa karibu na eneo la tukio, ili kutoa hifadhi kwa watu walioathiriwa. Eneo hilo linalofahamika kama Kiteezi, kwa miongo mingi limekuwa likitupwa taka taka za Kampala, hadi kugeuka na kuwa mlima, huku wakazi waishio karibu wakilalamika kutokana na taka zenye sumu, pamoja na uharibifu wa mazingira. Nchini Ethiopia, takriban watu 115 walikufa 2017 baada ya eneo la taka mjini Addis Ababa kuporomoka, huku wengine 17 wakifa 2018, mjini Maputo, Msumbiji, kwenye tukio sawa na hilo. – Reuters, AP, VOA #uganda #kampala #takataka #dumpo #maporomoko #vifo #polisi #voa #voaswahili
Idadi ya vifo katika eneo la kutupia takataka vyafikia 21
- 23 Oct 2024 - Israel on Tuesday confirmed it had killed Hashem Safieddine, the heir apparent to late Hezbollah leader Hassan Nasrallah who was killed last month in an Israeli attack targeting the Iran-backed Lebanese militant group.
- 23 Oct 2024 - A one-year-old child died while 14 passengers were hospitalised in serious condition after a truck rammed into a matatu along the Narok-Maimahiu road in the Pinyinyi area of Narok County on Tuesday night.
- 23 Oct 2024 - The E. coli outbreak, linked to one of McDonald's most popular menu items, has sickened 49 people and sent 10 to the hospital, officials say.
- 23 Oct 2024 - Germany has detected its first case of the new Mpox variant, the Robert Koch Institute for public health said on Tuesday, adding that it viewed the risk to the wider population as low.
- 23 Oct 2024 - Haitian gangs are ramping up attacks on areas they do not yet control, the head of the United Nation's Integrated Office in Haiti (BINUH) warned on Tuesday, after days of renewed violence from an alliance of armed gangs in the Caribbean nation.
- 23 Oct 2024 - South Africa sees Russia as a valued ally, President Cyril Ramaphosa said at a bilateral meeting with Russia's Vladimir Putin on Tuesday, on the eve of the BRICS summit of emerging economies that will take place in the Russian city of Kazan.
- 23 Oct 2024 - Paramilitary Rapid Support Forces have attacked villages in the east of Sudan's El Gezira state, killing at least 25 people, following the defection of high-ranking RSF officer Abuagla Keikal who is from the area, activists said.
- 23 Oct 2024 - The Kenyan government, through the Climate WorX program, has launched a transformative initiative to engage youth and women in environmental conservation efforts by establishing a mega tree nursery around Ngong Forest. The project aims to prepare 3,000…
- 23 Oct 2024 - The two sisters left their home in search of their mother who had visited a hospital.
- 23 Oct 2024 - Democratic U.S. Vice President Kamala Harris held a marginal 46% to 43% lead over Republican former President Donald Trump, with a glum electorate saying the country is on the wrong track, a new Reuters/Ipsos poll found.