- 352 viewsDuration: 1:48Waziri wa afya Aden Duale ametangaza nia ya serikali kupambana na visa vya akina mama na watoto kupoteza maisha yao katika vyumba vya kujifungua kidijitali. Akizungumza katika hafla ya nne ya kufuzu kwa mahafala wa mafunzo ya uuguzi katika hospitali ya rufaa na mafunzo ya Kenyatta (KUTRRH) Waziri Duale amedokezeza kuwa vituo vyote vya afya vitahitajika kutoa takwimu za kila siku na kuorodhesha sababu za akinamama au watoto kupoteza maisha yao katika vyumba vya uzazi kupitia mfumo wa kidijitali