- 229 viewsKwa kuenea kwa taarifa za uongo kwenye mitandao ya kijamii, waandishi wa habari nchini Msumbiji wako mstari wa mbele katika kupambana na upotoshaji na taarifa za uongo. Hapa katika chumba cha habari cha Evidencias, mjini Maputo, Msumbiji, Reginaldo Tchambule na timu yake wanafanya kazi ya kuweka rekodi sawa katika jitihada za kupambana na upotoshaji na taarifa za uongo. Yeye na mwenzake Nelson Mucandze, wanasema walianzisha pamoja gazeti na lile la mtandaoni miaka minne iliyopita kwa sababu mashirika mengine mengi hayakuwa yakikagua ukweli au kutumia taarifa na uchambuzi katika kuripoti kwao. Tchambule anasema hadhira yao ilianza kufuatilia kwa haraka. Reginaldo Tchambule, Evidencias Editor anaeleza: “Gazeti la Evidencias linaweza kuwa limepata muonekano na umaarufu mkubwa katika muda mfupi, kwa sababu ya jinsi tulivyozingatia uandishi wa habari wenyewe. Wakati fulani tulikuwa na ukurasa ambapo tulichunguza habari kuu zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii.” Mwaka huu, Tchambule aliripoti kwa nini Ossufo Momade, kiongozi wa Renamo, chama kikuu cha upinzani cha Msumbiji, hajaonekana hadharani kwa wiki kadhaa wakati wa kampeni za urais. Evidencias ilianza kuchunguza picha kwenye mtandao wa Facebook wa mgombea ambapo ilionekana Momade alikuwa akifanya kazi nje ya nchi. Ripoti ya Amarilis Gule VOA Maputo. #habaripotofu #msumbiji #maputo #chumbachahabari #Evidencias #gazeti #reginaldotchambule #voa #voaswahili
Nchini Msumbiji waandishi waongeza juhudi kukabiliana na habari potofu
- - 2025 SOYA Awards ››
- - 🔴 LIVE || TV47 ››
- 19 Apr 2025 - Canada's Prime Minister Mark Carney faced sustained attacks from his Conservative rival at an election debate Thursday, but the Liberal leader sought to focus attention on what he calls Canada's top threat, President Donald Trump.
- 19 Apr 2025 - Iran staged military parades on Friday to mark its annual Army Day celebrations, showcasing a wide array of its latest domestically built drones, missiles, tanks, and other hardware.
- 19 Apr 2025 - Top county officials summoned in waste firm deal
- 19 Apr 2025 - A woman is in custody after being found in possession of nearly 300 grams of cocaine, following a sting by a multi-agency security team targeting drug trafficking routes between Kenya’s Northern Frontier and the capital.
- 19 Apr 2025 - Idriss noted that the agency has observed a significant shift from development aid to investment-based financing, helping narrow the funding gap for well-prepared infrastructure projects.
- 19 Apr 2025 - After a 14-month hiatus, former Interior CS Fred Matiang'i, who left the country under a cloud of controversy after his home was raided by police, is back in the public sphere.
- 18 Apr 2025 - Gas blast kills two, injures several in Embakasi South
- 18 Apr 2025 - Detectives at the Kayole Police Station in Nairobi are holding a senior Imam for the offence of causing grievous harm to at least two persons.
- 18 Apr 2025 - Managing leg disorders in broiler chickens
- 18 Apr 2025 - Chaos erupted at the Kitale Museum on Friday afternoon as a modelling competition was violently disrupted by over 50 armed youths.