- 313 viewsDaktari wa Kipalestina Khaled al-Saedni anafanya kazi katika kitengo cha watoto cha hospitali ya Al-Aqsa Martyrs huko Gaza City. Daktari huyu, ambaye amefanya kazi katika hospitali hii kwa zaidi ya miaka 23, alipoteza mguu wake mwaka jana baada ya kujeruhiwa. Anasema alijeruhiwa na bomu katika kambi ya wakimbizi ya Al-Bureij katika miezi ya kwanza ya vita vya Gaza. Kutokana na matatizo yaliyotokana na maradhi ya kisukari, daktari huyu mwenye umri wa miaka 50 anasema, mguu wake ulikatwa. Lakini licha ya kutegemea kifaa cha kutembelea, daktari huyu wa watoto alisema amerejea kufanya kazi kuwahudumia watoto “katika fursa ya kwanza” aliyopata baada ya miezi kadhaa ya kufanyiwa upasuaji na kupata matibabu. “Nimepoteza mguu, namshukuru Mungu. Kuna watu familia zao nzima wamekufa shahidi – wake, watoto, wazazi na ndugu zao,” Saedni alisema, ana matumaini vita vya Gaza vitamalizika haraka. Israel ilianza mashambulizi ya angani na ardhini dhidi ya Gaza baada ya wapiganaji walioongozwa na Hamas kushambulia jamii za Waisraeli Oktoba 2023, na kuua watu 1,200 na kuwachukua mateka 250 kurejea nao Gaza, kulingana na hesabu za Isreali. Kampeni ya kivita ya Israeli tangu wakati huo imewauwa zaidi ya Wapalestina 46,500 na kuwajeruhi wengine zaidi ya 100,000, kulingana na wizara ya afya ya Gaza. Kampeni hiyo imewakosesha makazi watu milioni 2.3 na kuharibu eneo lote finyu la pwani. #ukandawagaza #daktari #khaledalsaedni #israel #mabomu #hamas #mateka #voa #voaswahili #kilema
Daktari
- 12 Mar 2025 - Water Cabinet Secretary Eric Mugaa has attributed the stalled construction of the Thwake multi-purpose dam at the confluence of Thwake and Athi rivers on the Kitui-Makueni counties border to the Russia-Ukraine war.
- 12 Mar 2025 - Atandi will be deputized by Dr. Robert Pukose following a hotly contested but decisive election.
- 12 Mar 2025 - The Pharmacy and Poisons Board (PPB) has cautioned manufacturers, distributors, wholesalers and healthcare facilities to store drugs according to the specified conditions following multiple complaints from the public over health concerns posed by low-…
- 12 Mar 2025 - The Commission for University Education has flagged 15 institutions for operating illegally in Kenya.
- 12 Mar 2025 - An investigation has been launched after a Kenya Forest Service officer allegedly shot a civilian dead at Kiptunga Forest in Kuresoi South on Tuesday evening.
- - Is the MMF party over?
- 12 Mar 2025 - The nine-month training at the Kiganjo Police Training College will now include a more in-depth curriculum.
- 12 Mar 2025 - The African Union (AU), through its Peace and Security Council (PSC), has condemned the announcement by the Rapid Support Forces (RSF) and its affiliated political and social forces of the establishment of a parallel government in the Republic of Sudan…
- 12 Mar 2025 - Despite KFS claims that the country’s forests are not at risk, evidence on the ground paints a different picture, with vast tracts being cleared, encroached upon, and allocated for projects that undermine Kenya’s environmental and climate commitments.
- 12 Mar 2025 - The first time Kevin Mutua heard of Attention Deficit Hyperactivity Disorder (ADHD), he was 21. It was not in a doctor’s office or a psychology class. It was on TikTok. He had spent most of his teen life being called ‘lazy’, ‘scatterbrained’, or ‘too…