Shirika la Utangazaji nchini KBC liliandaa siku yake ya kwanza ya maombi kwa lengo la kushukuru kwa baraka na ufanisi wa mwaka unaoisha na kutafuta mwongozo wa kiroho kwa ajili ya siku za usoni.Wakuu na wafanyakazi wa shirika la KBC walipata muda wa kuabudu pamoja na kusikiliza neno la Mungu pamoja na ushauri. Mkurugenzi Mkuu wa shirika hili, Agnes Kalekye, aliwapongeza wafanyakazi kwa bidii yao isiyoyumba na kujitolea katika kutekeleza majukumu yao licha ya changamoto nyingi wanazokabiliana nazo. Maombi hayo yalipangwa na Chama cha Waumini wa Kiprotestanti wa KBC, Jumuiya ndogo ya Waumini wa Kanisa Katoliki na Jumuiya ya Waislamu.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive