Mfanyakazi afikishwa kortini kwa kuiba pete ya Ksh 683,700 na kuiuza Ksh 4,000

  • | Citizen TV
    4,426 views

    Mfanyakazi mmoja wa nyumbani amefikishwa mahakamani kushtakiwa kwa wizi wa pete ya tajiri wake katika mtaa wa Runda hapa Nairobi. Violet Ndukwe Lijodi ameshtakiwa pamoja na Francis Mwima kwa wizi wa peke hiyo ya zaidi ya shilingi laki sita. Inaarifiwa kuwa Violet alipokuwa akifanya kazi katika mtaa wa Runda Acacia Grove aliiba na kumuuzia Francis pete hiyo kwa shilingi elfu nne pekee. Wameshtakiwa katika mahakama ya Milimani na wote wawili wakakana mashtaka.