Viongozi wa kidini katika kaunti ya Kiambu, kutoka mashirika mbalimbali ya kidini, wamekashifu matumizi mabaya ya mavazi ya kidini na umati wa watu waliokuwa wamebugia pombe, wanaodaiwa kuajiriwa na wanasiasa, kama ilivyoshuhudiwa hivi maajuzi huko Gatundu, Kaunti ya Kiambu. Wakizungumza katika eneo la Ruiru, walisema vurugu hizo katika mahali pa ibada zinaharibu heshima ya madhabahu. Wakati huo huo, katika kaunti ya Kakamega, askofu wa Kanisa Katoliki Joseph Obanyi anawaomba madereva kuwa makini barabarani wakati wa msimu huu wa sherehe za Krismasi.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive