Maelfu ya wakazi wa Kaunti ya Kajiado wanakabiliwa na hatari ya baa la njaa kufuatia ukame wa muda mrefu. Mamia ya wafugaji wamegura makwao kutafuta malisho na maji,huku maeneo ya Kajiado ya kati na Kajiado magharibi yakiwa miongoni mwa maeneo yaliyoathirika zaidi. Halmashauri ya kitaifa ya kudhibiti Ukame imeorodhesha Kajiado kuwa mojawapo ya maeneo yaliyoathirika pakubwa na ukame katika maeneo kame ,ambapo watu takriban 64,300 wanakabiliwa na uhaba wa chakula.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive