Rais Donald Trump ameanza utawala wake mpya wiki hii kwa kusaini mamia ya amri za kiutendaji kwa masuala mbali mbali kuanzia nishati hadi uhamiaji.
Baadhi ya amri zake ni pamoja na kufuta programu za mchanganyiko, uwiano na ushiriki na kutangaza kuwa serikali ya Marekani itatambua jinsia mbili tu – mwanamme na mwanamke.
“Kuanzia hivi leo, na kuendelea itakuwa ni sera rasmi ya serikali ya Marekani kuwa kuna jinsia mbili tu, mwanamme na mwanamke,” Trump alisema katika hotuba yake baada ya kuapishwa siku ya Jumatatu.
Siku moja baada ya kutangaza kuwa kutakuwa na jinsia mbili tu nchini Marekani na kusaini amri za kiutendaji ili kuwakamata wahamiaji haramu, Mchungaji wa Kanisa la Episcopal Mariann Edgar Budde alimrai Trump kuonyesha huruma kwa watu ambao walikuwa na hofu ya “kile” kitakacho tokea.
#trump #amriyakiutendaji #jinsia #reels #voa #voaswahili
12 Mar 2025
- Spain's government approved a bill on Tuesday imposing massive fines on companies that use content generated by artificial intelligence (AI) without properly labelling it as such, in a bid to curb the use of so-called "deepfakes".
12 Mar 2025
- Former Philippine President Rodrigo Duterte was arrested and taken into custody on Tuesday in Manila on an International Criminal Court warrant for the "war on drugs" that defined his term in office and which killed thousands of Filipinos.