Watu 100 ambao walikuwa wakichimba madini kinyume cha sheria katika mgodi wa dhahabu usiofanya kazi nchini Afrika Kusini walifariki baada ya kunaswa chini ya mgodi huo kwa miezi kadhaa, huku polisi wakijaribu kuwaondoa huko, kundi linalowakilisha wachimba migodi hao lilisema Jumatatu.
Sabelo Mnguni, msemaji wa jamii zilizoathiriwa na uchimbaji madini aliliambia shirika la habari la Associated Press kwamba simu ya mkononi iliyotumwa juu ya mgodi huo na baadhi ya wachimba migodi waliookolewa siku ya Ijumaa, ilikuwa na video mbili zikionyesha miili kadhaa iliyofunikwa kwa plastiki chini ya ardhi.
Mnguni alisema “takriban watu 100 walifariki katika mgodi katika mkoa wa kaskazini magharibi ambako polisi walianzisha operesheni mwezi Novemba kuwalazimisha wachimba migodi kuondoka.
Wanashuku watu hao walikufa kwa njaa au kwa sababu ya kukosa maji mwilini, Mnguni alisema.
Alisema miili 18 iliondolewa ndani ya mgodi huo tangu Ijumaa.
Msemaji wa polisi Brigedia Sebata Mokgwabone alisema bado wanachunguza taarifa kujua ni miili mingapi iliyopatikana na ni manusura wa ngapi waliookolewa baada ya operesheni ya uokoaji kuanzishwa Jumatatu.
-AP
#Stilfontein #madini #mgodi #dhahabu #wachimbaji #afrikakusini #wachimbajiharamu #voa #voaswahili
12 Mar 2025
- The rock went largely unnoticed for 20 years until the school, in Queensland's rural Banana shire, asked paleontologist Anthony Romilio to examine a cluster of three-toed track marks.
12 Mar 2025
- The first round notably eliminates the Office of the Chief Scientist, led by Katherine Calvin, a renowned climatologist who contributed to key UN climate reports. She and other US delegates were also barred from attending a major climate science meeting…
12 Mar 2025
- Spain's government approved a bill on Tuesday imposing massive fines on companies that use content generated by artificial intelligence (AI) without properly labelling it as such, in a bid to curb the use of so-called "deepfakes".
12 Mar 2025
- Former Philippine President Rodrigo Duterte was arrested and taken into custody on Tuesday in Manila on an International Criminal Court warrant for the "war on drugs" that defined his term in office and which killed thousands of Filipinos.